Tiba Asili Hatari Kwa Binadamu



nani.Na Veronica Romwald, Dar es Salaam
WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imesema zaidi ya asilimia 90 ya dawa za asili zilizofanyiwa uchunguzi kuhusu uwezo wake wa kutibu maradhi mbalimbali zimegundulika kuwa na kemikali zenye sumu ambazo ni hatari kwa binadamu.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake Dar es Salaam, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, alisema aina ya kemikali zenye sumu zilizogundulika kuwa kwenye dawa hizo ni pamoja na Alkaloid, Saponin na Anthroquinone.
Waziri Mwalimu alisema taarifa ya uchunguzi uliofanywa na Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali mwaka 2015/16, imeonyesha kuwa kati ya aina 95 za dawa zilizopokelewa na kufanyiwa vipimo ni asilimia saba pekee ndiyo iliyogundulika kuwa salama kwa matumizi ya binadamu.
“Ofisi ya Mkemia Mkuu ilipima aina 95 ya dawa hizo, asilimia saba tu ndizo hazikuwa na kemikali zenye sumu lakini kiasi kilichobaki kilikuwa na sumu lakini tunaona waganga hao hasa wa mijini wanaendelea kuzitumia kwa kuwapa wananchi jambo ambalo ni hatari,” alisema Waziri Mwalimu.
Alisema uchunguzi huo pia ulibaini kuwapo kwa kasoro nyingi kuhusu matumizi ya tiba za asili na kwamba waganga wengi hawajasajiliwa na Baraza la Tiba za Asili Tanzania.
Theme images by hanoded. Powered by Blogger.