MSHAHARA WA OKWI TISHIO

KILA mwenye nacho huongezewa, kwani Simba imemuongezea mshahara mshambuliaji wake Emmanuel Okwi ambaye sasa analipwa dola 4,000 kwa mwezi ambazo ni sawa na Sh milioni 7.Kabla ya ongezeko la mshahara huo, Okwi raia wa Uganda alikuwa analipwa mshahara wa dola 3,000 (Sh milioni 5.3).
Awali Okwi alikuwa akilipwa kiasi hicho cha fedha baada ya kujiunga na Simba akitokea Yanga ili kulinda kipaji chake, kwa mfumo wa kulipwa dola 2,000 kila mwezi na nyingine akiingizwa benki kwa muda wa miezi sita.Lakini mkataba mpya aliosaini hivi karibuni, Okwi analipwa dola 3,000 kila mwezi na dola 1,000 ameshalipwa ya mwaka mzima ili kusiwepo na malalamiko yasiyo ya lazima.

Emanuel Okwi akiwa na makamu wa Rais wa Simba Geofrey Nyange Kaburu


Bosi mmoja wa Simba, aliliambia Championi Jumamosi kuwa, hawana tabu na Okwi kwani analipwa kiasi hicho cha fedha na thamani yake inaonekana uwanjani.“Okwi analipwa dola 4,000, kati ya hizo 3,000 anapokea kila mwisho wa mwezi na ile 1,000 ameshapewa kwa muda wa mwaka mzima, hatuna tatizo naye,” alisema tajiri huyo mwenye sauti ndani ya Simba.
Chanzo hicho kilisema, mshahara huo mpya alianza kulipwa rasmi Januari, mwaka huu baada ya kusaini mkataba wake mpya wa mwaka mmoja.Okwi wakati anasaini mkataba wake, alilipwa fedha ya usajili dola 35,000 (Sh milioni 62) na nyingine dola 12,000 (Sh milioni 21) ambazo ni sehemu ya mshahara wake.
Kwa malipo ya mshahara anayopata Okwi, anakuwa mchezaji anayeongoza kwa msharahara kwa Simba na Yanga kwani Kpah Sherman wa Yanga analipwa dola 3,000 na Haruna Niyonzima wa timu hiyo analipwa dola 2,500 sawa na Sh milioni 4.8.
Hata hivyo, mshahara huo wa Okwi umezua manung’uniko kwa baadhi ya wachezaji wa Simba waliodai mwenzao anapendelewa kwa kila klabuni wakisahau kwamba kila kitu kinafanyika kwa makubaliano.



Wilbert Molandi na Sweetbert Lukonge,Dar es Salaam
Theme images by hanoded. Powered by Blogger.