Wazanzibar wanyonge wamjibu Maalim Seif

UKWELI KWA KATIBU MKUU WA CUF MAALIM SEIF NA WAPAMBE WAKE WA UKAWA KUHUSU HALI YA KISIASA ZANZIBAR

Ndugu Wananchi wa Zanzibar.
Kama tunavyoelewa kuhusu mazungumzo yanayoendelea baina ya Viongozi wetu wa kisiasa juu ya hali ya kisiasa Zanzibar.

Mazungumzo haya yalianza tangu mara baada ya kuahirishwa kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar kulikofanywa na ZEC baada ya kutokea kasoro mbali mbali.

Ndugu Wananchi
Katika kipindi hiki tunekuwa tukiona mambo, malumbano, vituko, na mabishano baina ya pande mbili za wafuasi wa vyama vya ccm na cuf. Lakini zaidi tuneona namna baadhi ya viongozi wakiwashutumu wenzao juu ya matendo na mwenendo wa viongozi hao. Kwa mfano tumeona hapa Katibu Mwenezi wa ccm alipotoa taarifa yake ya yaliyojiri katika kikao cha Kamati Maalum ya ccm Zanzibar, ghafla Jussa aliingilia kati na kusema kwamba hayakiwa ya ukweli, ukweli utapatikana baada ya mazungumzo kumalizika na viongozi wote watatoa kauli kwa pamoja.

Ndugu Wananchi,
Wote mnaelewa CUF wamesusia sherehe za Mapinduzi mwaka huu, Na pia mnaeleewa kwamba Maalim katika hangaika yake na ku overshadow sherehe hizi ameamua kuitisha mkutano na waandishibwa habari Dar asubuhi ya leo, kuzungumzia hali ya mazungumzo na mambo mengine.

Mimi nataka kumuuliza Jussa Ile kauli yake ya taarifa ya mazungumzo ya mwafaka aliyisema itatolewa na viongozi wote kwa pamoja mbona anakuja Bw Mkubwa wake tuu kuitoa??? Tena anaitilea kule kule kubaya na kwa wadhalimu Tanganyika???? Sisi tulitegemea angeliitolea Pemba tena Mtambwe... Nyumbani ni nyumbani na mcheza nyumbani mara nyingi huwa na baraka nyingi zaidi.

Ndugu Wananchi
Anachotaka kulizungumza Maalim Seif leo tunakijua na hakuna jipya zaidi ya mashairi yake ya Taarab kwamba apewe nchi.

1. Maalim anategemewa kuelezea namna mazungumzo yalivyokwenda na kutoridhika na hali ilivyo. Maalim alijua kwamba atakabidhiwa nchi kama walipanga na rafikie Amani Karume lkn kakwama kabisa amenginga ukuta. Kikao kimefikia maamuzi ya kurejewa kwa uchaguzi mapema mwezi February mwaka huuu. Hakuna siri juu ya hilo maatayarisha tayari watu wende chavda tuu kununua sare za Khanga kusubiri ushindi.
Jambo hili Maalim hajaliwafiki hivyo ameamua kukimbilia kwenye vyombo vya habari.

2. Wananchi leo Maalim Seif katika mkutano huu anataka kumfunika Dr Shein pamoja na Sherehe za Mapinduzi za kesho.... Hapa naomba mnielewe vizuri. Maalim anataka kutoa madai na hoja zake mbali mbali ambazo ameshatayatishiwa na akina Tundu Lisssu wanasheria wa Ukawa ili azitowe nje leo na kumfanya Dr Shei aonekane kama si Rais Halali hivyo kutia doa na dosari sherehe za kesho. Hili jambo limepangwa vyema na yeye Maalim ndie mtekelezaji baada ya kuomba kusaidiwa kufanya hivyo kwa akina mbowe na Mbatia. Sasa tusubiri mtaalamu Tubdu Lissu na wanasheria wenzake akina Awadh na othman Masoud wamemuandikia nini Bwana wao ili akizungumze leo.

3. Maalim atatoa kauli ya kutoshiriki uchaguzi na kuwaachia watu wake wafanye wanavyotaka ili wamsaidie kupata haki yake. Maana wanasema wamechoka wamechoka wamechoka na ccm waende The Hague. Hawajui kama The Hague ni kama kwenda ukweni siku ya ndoa lazima wende na sheikh na mashahidi. Ikiwa hoja ni huko nafikiri Cuf wanahitajika kufika mwanzo.

4. Maalim ameandaa mkutano pia kesho Zanzibar na viongozi wenzake wa Ukawa. hii inaonesha huyu bwana ameamua kugombana na wana mapinduzi.
Wakati wananchi wa Zanzibar wanashereheka Mapinduzi Maalim Seif anataka kukutana na viongozi wenzake wa ukawa na wafuasi wao Zanzibar. Hii yote ni kujaribu kuharibu taswira nzuri ya sherehe za mapinduzi ya Zanzibar kesho. Haiwezekani na haitiwezekana kwamba wananchi waliowengi wanasherehekea Uhuru wao halafu mahasidi wanakutana kuharibu Uhuru huo, nahisi kwa hapo patachimbika.

5. Mara baada ya mkutano wake wa leo. Cuf na Ukawa wameandaa makundi maalum ya kufanya fujo na uhalifu Zanzibar ili kutoa shindikizo la kutangazwa Maalim. Hili ni siri ya maalim na ukawa wenziwe lakini anachokitaka Maallim nikuonekana wana cuf wanadai Serikali yao kwa kupitia fujo na uvunjajibwa amani.

6. Maalim asubuhi ya leo anatarajiwa kutangaza kwamba Hatoshiriki marudio ya uchaguzi wa Zanzibar kwa vile yeye ni mshindi kama anavyodai. Suala hili linatokana na Maalim kugonga ukuta lila anakokimbilia anaelezwa kwamba lazima arejee uchaguzi, suala ambalo halitaki hata kulisikia.

Mimi siamini ninachokiona kwasababu kama duru ya mwanzo anavyodai maalim kashinda majimbo tisa na urais juu basi angeliweza kurejewa uchaguzi na kuweza kushinda tena. watu wale wale waliompigia kura wapo na watampa tena. wasiwasi wa nini??

MWISHO
Tunamuambia Maalim Seif aendelee kukutana na waandishi sisi sherehe zinaendelea kama kawaida na wala hana ubavu wa kuziharibu sherehe zetu, tupo makini. wala hana ubavu wa kuharibu hotuba ya Rais wetu wala Mood za wana ccm tuko ngangari kama 12 Jan1964. Tupo tayari kwa lolote. Jeshi letu, Serikali yetu, Mahakama zetu, Magereza yetu na hata wewe Maalim tunakuea sie basi hayaaa tuine yanavyokwenda baba.

Kwa taarifa tuu Wananchi na Maalim kwa ujumla ZEC imeshaamua na inajioanga kufanya marejeo ya uchaguzi, Maalim ukigoma sisi tunakwenda mbele. Vyama vyengine vipo vitashiriki na bahati nzuri kwa muono wetu wa haraka VP1 atakuwa Mhe Hamad Rashid.

Ingawa hutaki hata kumuona. unamchimba kwa kila hali Maalim kwa nini? Wewe na ukawa wenzio mnamtumilia Said Miraji wa ADC kumsumbua Hamad Rashid kawakosa nini??? Kwasababu anataka ADC ishiriki uchaguzi na nyinyi hamtaki? Maana Maalim msimamo wa ukawa ni kwamba hata uchaguzi ukitangaziwa basi mufanye fujo usiwe wa amani na usiwezekane.

Maana kufanyika na kufanikiwa kwa uchaguzi wa marejeo ni PIGO kwa Cuf, Chadema, NCCR kwa ujumla upinzani utakuwa umepata pigo kubwa. na hilo hamkobtayari kuliona. mko tayari kuona damu inamwagika kwa uchu wa madaraka. mko tayari kuona UN ndio inakamata uendeshaji wa Serikali. mnachrkrsha kweli kweli nyie watu. Hivi Tanzania haina uwezo hadi UN wafike kutusaidia kuendesha mambo yetu. Bado mna akili za kutawaliwa hadi leo miaka 52 ya mapinduzi?

Maalim tumepata taarifa kwamba hata wafuasi wenu Mabalozi wa nje waliopo Tanzania wamekpeni fedha ili mvinunue vyama vidogo vya siasa visishiriki uchaguzi wa marudio. Mtoaji pesa tunamjua. mkamataji na waratibu wako wa shughuli hiyo tunawajua na tunakwambia tutawashughulikia wote Bara na Zanzibar maana hili suala lina interest mpaka za Mbowe. Lowassa na Mbatia. Kwa tamaa yao wanahisi cuf ikipata Zanzibar kwa wao itakuwa Raus kuipata Tanzania Bara.

Bado mnaota ndoto za mchana. Tunajua waraka huu Maalim utaupata kabla ya Pree Conference yako ili ukusaidie kuipanga vyema taarifa yako na pengine kuifumua upya maana siri zimevunja na watoaji wako wa siri ni wake wale wasaidizi wako karibu wenye tamaa ya fedha tulioweza kuwanunua kwa bei ya tonge kwa tonge.

Maalim pamoja na kususia sherehe zetu tunakutakia kila la kheri katika kusherehekea kimoyomoyo. sisi waliowengi tunashiriki.

Wasalaaam
Wako
Mtandao wa wanyonge waliowengi Zanzibar
 Via Jamii Forum
Theme images by hanoded. Powered by Blogger.