Uporaji wa fedha kwa bodaboda watikisa Dar

Matukio ya uporaji na mauaji kwa kutumia pikipiki  yanazidi kushika kasi na kusababisha hofu kubwa kwa wananchi na wafanyabiashara jijini Dar es Salaam pindi wanapotoka benki, wanaposafirisha fedha kutoka eneo moja kwenda jingine au kufanya manunuzi.
 
Uchunguzi wa Nipashe umebaini kuwa, uporaji huo unaofanywa na majambazi kwa kutumia pikipiki hasa aina ya Boxer una mtandao mkubwa wa wahusika kutoka hatua ya kwanza ya mtu anapochukua fedha iwe benki au sehemu nyingine yeyoye hadi tukio zima la kuporwa linapotokea.
 
Jana watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi katika eneo la Mikocheni, jijini Dar es Salaam walimuua Conrad Kamukara, kwa kumpiga risasi akiwa anaelekea ofisi za kampuni ya Nabaki Afrika kununua vifaa vya ujenzi.
Theme images by hanoded. Powered by Blogger.