SERIKALI YA KOMAA NA TIBA MBADALA
TAMKO la Serikali kuhusu matangazo ya Tiba Asili na Tiba Mbadala, limesisitizwa kwamba liko palepale kwa kuwa lengo ni kuboresha huduma hiyo.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema hayo alipokuwa anazungumzia juu ya kuhusu hilo juzi jijini Dar es Salaam.
Katika tamko lililotolewa Desemba 24, mwaka huu Serikali imepiga marufuku matangazo yote yanayohusu tiba asili na tiba mbadala kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii. Kwa mujibu wa tamko hilo, wenye vibali wametakiwa kuviwasilisha pamoja na matangazo yao kwenye Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala, ili vifanyiwe mapitio.
Tamko hilo limefafanua kuwa utoaji wa elimu ya afya kwa umma unaofanywa na watoa huduma za tiba asili na tiba mbadala kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, umepigwa marufuku hadi hapo utaratibu mwingine utakapotangazwa.