KUTANA NA SHULE YENYE WANAFUNZI 45 TU KUTOKA KIDATO CHA KWANZA MPAKA CHA NNE

 Shule ya Sekondari Panzua iliyoko kata ya Panzua Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, ina jumla ya wanafunzi 45 wa kidato cha kwanza hadi cha nne.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu kutoka wilayani humo, Ofisa Kilimo wa kata hiyo, Muharami Makulika, alisema wanafunzi hao wanatoka katika vijiji saba vinavyoizunguka kata hiyo. Alivitaja vijiji hivyo kuwa ni Kibuyuni, Mkuruwili, Masanganya, Bupu kwa Wilaya ya Mkuranga na Kisarawe kijiji cha Malegele na Bwama.
 
Alisema takwimu za mwaka jana zinaonyesha shule hiyo ilikuwa na idadi ya wanafunzi 50 tu katika kidato cha kwanza hadi cha nne, jambo linalosababisha kufa kwa elimu katika kata hiyo, huku wengi wao ambao ni wa kike wakidaiwa kuolewa katika umri mdogo kutokana na wazazi na walezi kushindwa kuwasomesha.
Theme images by hanoded. Powered by Blogger.