KUTANA NA SHULE YENYE WANAFUNZI 45 TU KUTOKA KIDATO CHA KWANZA MPAKA CHA NNE
Shule ya Sekondari Panzua iliyoko kata ya Panzua Wilaya ya Kisarawe
mkoani Pwani, ina jumla ya wanafunzi 45 wa kidato cha kwanza hadi cha
nne.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu kutoka wilayani humo,
Ofisa Kilimo wa kata hiyo, Muharami Makulika, alisema wanafunzi hao
wanatoka katika vijiji saba vinavyoizunguka kata hiyo. Alivitaja vijiji
hivyo kuwa ni Kibuyuni, Mkuruwili, Masanganya, Bupu kwa Wilaya ya
Mkuranga na Kisarawe kijiji cha Malegele na Bwama.
Alisema takwimu za mwaka jana zinaonyesha shule hiyo ilikuwa na
idadi ya wanafunzi 50 tu katika kidato cha kwanza hadi cha nne, jambo
linalosababisha kufa kwa elimu katika kata hiyo, huku wengi wao ambao ni
wa kike wakidaiwa kuolewa katika umri mdogo kutokana na wazazi na
walezi kushindwa kuwasomesha.