CUF - RAISI ASITEUE VIONGOZI WA ZEC
Wamesema haiwezekani Rais kupewa uwezo wa kuteua viongozi wa Nec
wakati yeye ni sehemu ya mgombea wa urais pamoja na chama chake kuwa
sehemu ya mshiriki wa uchaguzi huo. Msimamo huo ulitolewa na Mkurugenzi
wa Mipango na Uchaguzi wa Chama hicho, Omar Ali Shehe, katika mahojiano
maalum na Nipashe mjini hapa kuhusu mkwamo wa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar.