Kubenea Akana Kumtukana Dc Makonda


Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (44) amekana kumtukana Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda tarehe 14 Desemba 2015 walipokutana katika Kiwanda cha Tooku Garments Co. Ltd. kilichopo eneo la External Mabibo kwa madhumuni ya kutatua mgogoro kati ya wafanyakazi na uongozi wa kiwanda hicho

Katika kesi inayosikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, Wakili wa Serikali mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa alimsomea mshtakiwa maelezo ya kesi hiyo ambapo baadhi  ya mashtakiwa aliyakana.
Theme images by hanoded. Powered by Blogger.