Kubenea Akana Kumtukana Dc Makonda
Mbunge
wa Ubungo, Saed Kubenea (44) amekana kumtukana Mkuu wa wilaya ya
Kinondoni, Paul Makonda tarehe 14 Desemba 2015 walipokutana katika
Kiwanda cha Tooku Garments Co. Ltd. kilichopo eneo la External Mabibo
kwa madhumuni ya kutatua mgogoro kati ya wafanyakazi na uongozi wa
kiwanda hicho
Katika
kesi inayosikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, Wakili
wa Serikali mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa alimsomea mshtakiwa maelezo
ya kesi hiyo ambapo baadhi ya mashtakiwa aliyakana.
