Kinondoni kujenga sekondari 6 wiki ijayo

 
WILAYA ya Kinondoni imeazimia wiki ijayo kuanza kujenga shule sita za sekondari katika kata zote ambazo hazina sekondari. Hatua hiyo imelenga kuwezesha wanafunzi 3,000 ambao wamefaulu mtihani wa darasa la saba na kukosa nafasi za kujiunga na kidato cha kwanza mwakani, wajiunge na masomo ya sekondari.
Mkuu wa wilaya hiyo, Paul Makonda, alisema hayo jana na kuzitaja kata zisizo na sekondari kuwa ni Mzimuni, Ubungo, Kimara, Kinondoni, Magomeni na Mbezi Juu. Alisema kukosekana kwa shule katika kata hizo husababisha wanafunzi wanaofaulu katika kata hizo kukosa nafasi au kupangiwa shule zilizo mbali na makazi yao.
Alisema kitendo cha wanafunzi hao kupangiwa shule za mbali kunawafanya kukumbana na adha mbalimbali za usafiri na kukosa umakini katika masomo yao na kuwaweka katika mazingira hatarishi. Mwaka huu wanafunzi 3,183 wamekosa nafasi za kujiunga na kidato cha kwanza.
Theme images by hanoded. Powered by Blogger.