MSIGWA, LISSU, LEMA NA PROFESA J KUTIKISA IRINGA MCHANA WA LEO




WAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM) kikitarajiwa kufanya mkutano wake mkubwa kesho jumapili katika viwanja vya Mwembetogwa mjini Iringa, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) leo Jumamosi kinatarajiwa kufanya kufuru katika uwanja huo huo.

Mkutano huo ulioandaliwa na Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) unatarajiwa kuwashirikisha viongozi mbalimbali vinara wa chama hicho.

Mbali na Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, wengine wanaotarajiwa kuhutubia katika mkutano huo ambao maandalizi yake yamekwishakamilika ni pamoja na Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, Mbunge wa Arusha Godbless Lema na Msanii wa kizazi kipya ambaye hivikaribuni ametangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo la Mikumi, Profesa J.

Tofauti na mikutano mingi ambayo kimekuwa kikifanya mjini hapa, safari hii, labda kutokana na ujumbe mzito, chama hicho kitatumia jukwaa la kisasa ambalo halina tofauti na majukwaa yanayotumiwa katika shughuli kubwa za kisanii nchini.


Leo na kesho wakazi wa Iringa wanatarajia kusikiliza sera za vyama hivyo vya Chadema na CCM ikiwa imebaki miezi michache kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani.
Theme images by hanoded. Powered by Blogger.