Bodaboda wapewa kichapo cha mbwa mwizi kutoka kwa wananchi wenye hasira kali baada ya kukwapua mkoba
Mmoja kati ya vibaka hao akiwa hoi baada ya kupata kichapo kikali.
Vijana wawili wa bodaboda ambao majina yao hayakuweza kupatikana mara moja, hivi karibuni walikoswakoswa kuuawa baada ya kupora mkoba uliokuwa na simu ya mwanamke aliyekuwa akipita njia.
Tukio hilo lilijiri Jumanne iliyopita, saa 1.30 usiku maeneo ya Sinza Afrikasana, pembeni mwa Baa ya Hongera ambapo inadaiwa ni eneo hatari kwa wizi huo.Shuhuda wa tukio hilo alilitonya gazeti hili kuwa, imekuwa ni tabia kwa baadhi ya vijana kutumia usafiri wa bodaboda kupora watu simu na mikoba hasa wanawake na kwamba siku hiyo arobaini ya vijana hao ilikuwa imefika.
Askari polisi akiwa katika eneo la tukio.
“Yaani ilikuwa ni Mungu tu maana bodaboda isingegoma kuwaka, tusingewapata. Basi raia wenye hasira kali wakaanza kuwashushia kipigo, aliyekuwa akiendesha pamoja na yule dada aliyeibiwa wakachukuliwa hadi Kituo cha Polisi Mabatini huku aliyekwapua akipewa kipigo,” alisema shuhuda huyo.
Bodaboda iliyokuwa inatumiwa na vibaka hao ikiwaka moto baada ya kuchomwa na wananchi wenye hasira kali.