Huu ni utengenezaji wa video ya wimbo wa Christian Bella aliowashirikisha Weusi ?




Mwishoni mwa mwaka jana mkali wa masauti Christian Bella aliachia ngoma mbili alizowashirikisha Alikiba na Koffie Olomide lakini haoneshi dalili za kupunguza mwendo.

Sasa ni zamu ya Weusi na huenda tayari wameshoot video yake. Bella aliingia kwenye studio za The Industry ya Nahreel kurekodi wimbo na Joh Makini na G-Nako October mwaka jana.

Joh Makini ameshare picha inayoonesha kuwa wako location kushoot video hiyo.
Theme images by hanoded. Powered by Blogger.