UKAWA WASUSIA UCHAGUZI WA KAMATI ZA BUNGE

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimefanikiwa kuchukua nafasi nyingi za wenyeviti na makamu wake baada ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi wa  kamati Bunge katika uchaguzi uliofanyika leo.


Hawa ndio wenyeviti  na makamu wake katika kamati  hizo, Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) Mwenyekiti atatoka  vyama vya upinzani ambapo bado  hajafahamika ila Makamu wake  ni mbunge wa Mwibara Kangi Lugola (CCM).

Waliochaguliwa katika kamati nyingine ni pamoja na mbunge wa Kigoma Kaskazini Peter Serukamba (CCM) ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, na Makamu wa wake ni Mbunge wa Busega Raphaeli Chegeni (CCM).

Kamati ya Sheria ndogo itaongozwa na Mbunge wa Bariadi Magharibi Andrew Chenge (CCM) na makamu wake ni mbunge wa Sengerema William Ngeleja (CCM)

Kamati ya Nishati na Madini mwenyekiti ni mbunge wa viti maalum CCM mkoa wa Singida Martha Mlata na makamu wake ni mbunge jimbo la Chumbuni Ussi Pondeza (CCM).

Kwa mujibu wa kanuni za Bunge mwenyekiti wa kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) anatakiwa kutoka upinzani hivyo bado hajachaguliwa. Kwa upande wa   makamu wake aliyechaguliwa ni mbunge wa Sumbawanga Mjini Aeshi K. Hilary (CCM).

Wakati uchaguzi wa wenyeviti  wa Kamati za Bunge ukifanyika taarifa zilizotufikia katika mtandao huu ni kwamba Wabunge wote wa Upinzani wamegoma kushiriki katika uchaguzi huo kwa madai kuwa umefanywa bila kuzingatia masuala muhimu.
Theme images by hanoded. Powered by Blogger.