SIKU NNE SHUBIRI KWA SERIKALI BUNGENI
Zilikuwa siku nne ngumu kwa Serikali bungeni. Ndivyo unavyoweza kuelezea hali ilivyokuwa kwenye chombo hicho cha kutunga sheria katika siku za mwanzo za mkutano wa pili wa Bunge la Kumi na Moja.
Mkutano huo ulioanza Jumanne, ulikumbwa na mlolongo wa maombi ya mwongozo kuhusu uamuzi wa kituo cha televisheni cha Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kupunguza matangazo ya moja kwa moja ya shughuli za Bunge.
