Maalim Seif Kupasua Jipu Leo
Hii ni
habari inayopewa nafasi ya kwanza na mtandao wa Jamjicho Blog.Maalim
Seif ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Katika sintofahamu iliyopo sasa kwa muda mrefu hajanukuliwa akitoa kauli. Tayari msimamo wa CCM Zanzibar umefahamika, kuwa wako tayari uchaguzi urejewe. CUF wao wanasikika wakiweka msimamo kuwa wao ndio washindi, watangazwe tu.
Katika sintofahamu iliyopo sasa kwa muda mrefu hajanukuliwa akitoa kauli. Tayari msimamo wa CCM Zanzibar umefahamika, kuwa wako tayari uchaguzi urejewe. CUF wao wanasikika wakiweka msimamo kuwa wao ndio washindi, watangazwe tu.
Katika
hili wa kutangaza hilo ni Tume, na ni Tume hiyo hiyo iliyoyafuta matokeo
na maamuzi kuchapwa kwenye gazeti la Serikali. Hilo likitoa tafsiri
kuwa Tume haiwezi katika mazingira ya sasa kuyapitia upya maamuzi ambayo
inadai yamefanyika kisheria.
Maalim
Seif kwa kuongea na Wahariri leo anamtangulia njiani Dr Shein kwa hotuba
yake ya kesho kwa Wazanzibar kupitia maadhimisho ya sherehe za
Mapinduzi. Kauli ya Maalim Seif leo itatoa mwanga wa Wazanzibar
wanakokwenda.
Tumepata
kulitolea maoni hili, kuwa, katika mazingira ya sasa, hekima na busara
ikitangulizwa, hakuna namna yeyote ile nyingine kwa Wazaznibar kusonga
mbele bila kukubaliana kwa pamoja, kuwa wanarejea uchaguzi chini ya
taratibu na uangalizi usio tia mashaka ya pande mbili kuchezeana rafu
mbaya. Matokeo ya uchaguzi kwenye uchaguzi huo lazima yaheshimiwe na
pande zote mbili na yatapelekea kuunda Serikali nyingine ya Umoja wa
Kitaifa, maana, kwa Zanzibar ilivyo sasa, na kwa Katiba yao mpya
inavyoruhusu, muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa- GNP ni tiba
mujarab kwenye yenye kuwasibu Wazanzibar.
