LEMBELI ATOA KAULI NZITO BAADA YA RAIS MAGUFULI KUMTEMBELEA SUMAYE HOSPITALINI


MBUNGE wa zamani wa Kahama kwa tiketi ya CCM kabla ya kuhamia Chadema,James Lembel ameibuka na kudai kuwa haikuwa na maana kwa Rais Magufuli kumtembelea Waziri Mkuu wa zamani Fredick Sumaye aliyelazwa katika Hospitali ya Muhimbili wakati alikuwa katika uangalizi mzuri zaidi wa kidaktari tena akiwa anapatiwa huduma zote muhimu.
Badala yake,Lembeli ambaye alishindwa vibaya katika kinyang'anyiro cha kuwania Ubunge katika Jimbo la Kahama Mjini.amesema kuwa ni vema Rais Magufuli angeenda kuwajulia hali wahanga wa bomoa bomoa ili kujua hali zao na jinsi ya kjuwasaidia. 
James Lembeli - Chadema
Politician · 11,024 Likes
 · 13 hrs · 
Ni vema kuona mgonjwa, ila ana wauguzi na kitanda kizuri. Inaleta maana zaidi kutembelea waliovunjiwa nyumba na dola ili kuona wanapolala kwa sasa na kuwashika mkono.
Theme images by hanoded. Powered by Blogger.