KESI YA KUBENEA IMEFIKIA HAPA
Mbunge wa Ubungo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Saed Kubenea.
Hatua hiyo ilifikiwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba
baada ya upande wa Jamhuri kudai kuwa kesi hiyo ilipangwa kusikilizwa
jana lakini shahidi hakufika mahakamani hapo.
Wakili wa Serikali Mwandamizi Credo Lugaju alidai kuwa kesi
ilipangwa kusikilizwa Januari 20 na 21, mwaka huu, ushahidi wa Jamhuri
lakini upande wa Jamhuri haukuwa na shahidi na uliomba tarehe nyingine
ya kusikiliza.
Hata hivyo, wakili wa utetezi Peter Kibatala alidai kuwa mshtakiwa
anatakiwa kuhudhuria vikao vya kamati za bunge mjini Dodoma, aliomba
kesi hiyo ipangwe mwezi Februari.
Hakimu Simba alisema kesi hiyo itaanza kusikilizwa Februari 8 na 9, mwaka huu na dhamana ya mshtakiwa inaendelea.
Katika kesi ya msingi, Kubenea anadaiwa kuwa Desemba 14, 2015,
katika Kiwanda cha nguo cha TOOKU kilichoko Mabibo External, Dar ves
Salaam, Kubenea alitumia lugha ya matusi dhidi ya Mkuu wa Wilaya ya
Kinondoni, Paul Makonda, hali ambayo ingeweza kusababisha uvunjifu wa
amani.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa Kubenea alimwambia Makonda; “wewe
kibaka, mpumbavu, mjinga na cheo chenyewe cha kupewa tu,” ulinukuu
upande wa Jamhuri.
CHANZO:
NIPASHE