DIWANI KILOSA AVUNJA KAMATI YA MAJI
Diwani wa kata ya Magole wilayani Kilosa mkoani Morogoro Alfat Saidi
amelazimika kuvunja kamati ya maji kutokana na kushindwa kufikia malengo
ya makusanyo ya fedha za mradi wa maji kiasi cha shilingi milioni kumi
na nne laki nne kwa mwaka na badala yake kukusanya zaidi ya shilingi
milioni moja na laki mbili tu kwa miaka mitatu.