MVUA YALETA MAAFA HUKO ZANZIBAR

Paa la jengo la Beit-al-ajab moja ya kivutio kikubwa cha utalii Zanzibar limeanguka na kusababisha mtafaruku mkubwa kwa wakazi wa Mjimkongwe.
Paa hilo limeanguka baada ya kuwepo mvua na upepo mkali ambao ulianza wakati wa asubui na paa hilo lilioko kwenye jengo hilo la ghorofa tatu kuanguka chini na kuharibu gari tatu zilizokuwa zimeegeshwa huku mshutuko huo ulisababisha watu kukimbia na kuacha mali zao za biashara hata hivyo hakuna atahri za kuumia binadamu.
 
Wakiongea na Mtandao huu baadhi ya mashuuda walioshuudia paa hilo likianguka wamesema ajali hiyo ilitokozea ghafla na kilichosaidia na kwanza kuwepo kwa sauti ya mshtuko na baadaye ndio paa hilo likaanza kuanguka hali hiyo ndiyo iliyosaidia watu waliokuwa wameketi chini na wafanyabiashara za watalii.
 
Naye mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya hifadhi wa Mjimkongwe Zanzibar Bw Issa Sarboko akiongea na Mtandao wetu kwenye eneo la tukio amesisitiza kuwa jengo hilo ni madhubuti na halijaathirika kilichotokozea ni kuwepo mwanya wa upepo lakini mamlaka inalishugulikia ili kuondosha tatizo lakini kwa hivi sasa jengo ilo limefungwa kwa ajli ya ukarabati.
 
Jengo hilo la Beita ajab ambalo ni moja ya kivutio kikubwa cha watalii Zanzibar, hii ni mara ya pili ya kuwepo kwa ajali za kuporomoka kwa jengo hilo ambalo limekuwepo zaidi ya miaka 100 na lilikuwa ni jengo la ofisi kuu za serikali kabla ya mapinduzi na hivi sasa ni makumbusho kubwa la historia ya Zanzibar.
 
source: Itv
Theme images by hanoded. Powered by Blogger.