POLISI WAMUOKOA MSUVA TAIFA


 Simon Msuva akisindikizwa na askari kupanda usafiri wa kumuondoa eneo la uwanja wa Taifa jana baada ya mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kati ya Yanga na Simba, uliomalizika kwa Yanga kufungwa bao 1-0, na kufanya mashabiki kumzingira wakitaka kumpiga wakimtuhumu kuuza mechi hiyo na kucheza chini ya kiwango.
*********************************************
Na Ripota wa Sufianimafoto, Dar
MCHEZAJI wa Yanga, Simon Msuva, amenusurika kupewa kichapo kutoka kwa mashabiki wake na kuokolewa na Polisi, baada ya mchezo wa jana kumalizika.

Msuva, aliyekuwa wa mwisho kutoka ndani ya vyumba vya kubadilishia nguo, huku wachezaji wenzake wote wakiwaa tayari wameshaingia ndani ya basi lao, alizongwa na mashabiki huku wakimsemea maneno makali na kutishia kumtwanga wakidai kuwa ameuza mechi.

Winga huyo, aliokolewa na Polisi walioanza kuwatawanya mashabiki hao kwa virungu, huku wengi wakimshika mkono Msuva na kumuweka kati ili kumfikisha kwenye usafiri ili kuondoka eneo hilo.

Askari hao pia walionekana kuchanganyikiwa huku wakimuongoza mchezaji huyo, kuelekea pasipojulikana huku wakitafuta basi la timu wakati tayari walishalipita na likiwa na ukubwa ambao kamwe huwezi litafuta kama gari ndogo.

Vurugu hizo ziliendelea huku mashabiki wakimfuata Msuva, wakimtukana huku pia askari hao wakijitahidi kuwatawanya kwa virungu, wakiendelea kutafuta basi la timu hadi alipofika Salum Telela na kumshika mkono kumuelekeza basi lilipo na kuelekea katika basi akiwa chini ya ulinzi.


Baada ya Msuva kupanda basi hilo lilianza kuondoka mahala hapo mashabiki wakilifukuza huku wakiendelea kutukana matuzi na kumtuhumu Msuva kwa maneno kuwa ‘eti’ ameuza mechi.
 Chini ya ulinzi mkali.
 Wakitafuta Basi la wachezaji 
 Mashabiki wakimzonga Msuva
 Wakirejea kupanda basi la wachezaji baada ya Telela kumfuata na kumwonyesha basi lilipo.
 Wakielekea kwenye basi hilo.
Wakimpandisha basi
Theme images by hanoded. Powered by Blogger.