AZAM FC WATWAA UBIGWA ZAMBIA
Sare hiyo imeifanya Azam FC kufikisha jumla ya pointi tano sawa na washindi wa pili Zanaco, lakini imewazidi washindi wa pili hao wa Ligi Kuu Zambia, kwa wastani wa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.
Azam FC kama ingekuwa makini kwenye mchezo huo huenda ingejiandikia bao la uongozi dakika ya 8 baada ya kufanya shambulizi kali langoni mwa Zanaco, lakini shuti alililopiga Kipre Tchetche nje kidogo ya eneo la 18, lilipanguliwa na kipa na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda.